Wamiliki wa Costa Concordia kulipa fidia

Imebadilishwa: 27 Januari, 2012 - Saa 13:39 GMT

Wamiliki wa meli moja ya kifahari iliyozama katika pwani ya magharibi ya Italia mapema mwezi huu, wametangaza kuwa wako tayari kuwalipa fidia abiria wote waliokuwa kwenye meli hiyo.

Kwa mujibu wa ripoti, kila abiria atalipwa dola elfu kumi na tano. Haya yanajiri baada ya majadiliano kati ya mashirika kadhaa ya kutetea maslahi ya wateja nchini Italia.

Fedha hizo ni fidia kwa abiria ambao walipoteza mali yao na pia kuathirika kiakili. Hata hivyo mkataba huu haushirikishi watu waliopoteza jamaa wao katika mkasa huo au wale waliojeruhiwa.

Miili kumi na sita tayari imepatikana kutoka kwa mabaki ya meli hiyo ijulikanayo kama Costa Concordia.

Watu wengine kumi na sita hawajulikani waliko.

bbc.co.uk navigation

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.