Goodluck ataka Boko Haram kujitambulisha

Imebadilishwa: 27 Januari, 2012 - Saa 07:57 GMT

Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria amewataka viongozi wa kundi la wapiganaji wa kiislam la Boko Haram, kujitokeza hadharani na kutangaza wanachotaka kama njia ya kufungua majadiliano na serikali.

Amesema makabiliano ya kijeshi pekee hayatasaidia kumaliza mashambulio ya kigaidi ambayo yanatishia usalama wa nchi hiyo.

Rais huyo amesema ikiwa hawatajitambulisha basi hakuwezi kufanyika majadaliano yoyote na kundi hilo.

Tamko hilo la Goodluck linakuja baada ya kiongozi wa Boko Haram kukanusha kuwa walihusika na mashambilizi ya hivi karibuni katika mji wa Kano uliosababisha vifo vya watu 185.

bbc.co.uk navigation

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.