Skip to main contentAccess keys helpA-Z index
BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 28 Aprili, 2010 - Imetolewa 03:05 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Uchaguzi wa Sudan waendelea kuzua utata
 
Kiongozi wa chama cha upinzani cha pili kwa ukubwa huko Sudan Kusini ameieleza BBC kuwa kulikuwa na vitendo vingi vya ukiukwaji wa sheria katika uchaguzi wa kihistoria uliofanyika hivi karibuni.

Lam Akol, mkuu wa SPLM-Democratic Change, na viongozi wa vyama vingine vinane vya Sudan Kusini wameamua kwenda mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi.

Salvir Kiir, kiongozi wa chama cha Sudan People's Liberation Movement (SPLM), alipata ushindi wa asilimia 93 ya kura zote za kusini.

Mpinzani wake pekee alikuwa Bw Akol - ambaye anachukuliwa kuwa anawakilisha maslahi ya serikali kuu ya Sudan Kaskazini.

Malalamiko

Bw Akol alimweleza mwandishi wa BBC, James Copnall, mjini Khartoum kuwa anataka mahakama zibatilishe na kutengua matokeo ya kusini kwasababu uchaguzi ulitawaliwa na udanganyifu na kwamba matokeo hayo hayawakilishi maoni ya wananchi.

"Ukweli uko wazi kabisa," alieleza.

"Mgombea [Bw Kiir] kupata asilimia 93 ya kura ni jambo halijawahi kutokea katika mchakato wa kidemokrasia.

"Pia ni ushahidi kuwa kuna udanganyifu mkubwa."

Bw Akol alidai kuwa wakati wa upigaji kura majeshi ya usalama ya SPLM yalichukua udhibiti wa vituo vya kupigia kura, waliwatisha na kuwanyanyasa wapiga kura, na kukamata wawakilishi wa vyama vya upinzani.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha