Skip to main contentAccess keys helpA-Z index
BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 17 Machi, 2010 - Imetolewa 19:22 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
UN Habitat: Makazi bado ni tatizo duniani
 
Shirika la Umoja wa Mataifa la makazi duniani, UN Habitat, limetoa ripoti inayozungumzia tabaka lililopo katika miji kwa wakazi wenye kipato kikubwa na wale walio na kipato duni.

Tabaka hilo ni kubwa na linatishia ubora wa miji mbalimbali duniani na hali ya wakazi wake hasa wenye kipato duni.

Ripoti hiyo itakuwa ni ajenda kuu itakayojadiliwa katika Kongamano la tano la mipango miji duniani, litakalofanyika mjini Rio De Jenairo, Brazil hivi karibuni.

Akizungumza mjini London, mkurugenzi mtendaji wa shirika la makazi duniani, UN Habitat, Profesa Anna Tibaijuka alieleza kuwa nchi za kusini mwa jangwa la Sahara zinahitaji kufanya marekebisho makubwa ya sera zao za makazi na kuzitekeleza.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha