Skip to main contentAccess keys helpA-Z index
BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 19 Novemba, 2009 - Imetolewa 13:07 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Askari wa Mugabe waondoka migodini
 
Zimbabwe imesema inawaondoa askari wake kwenye migodi ya almasi mashariki mwa nchi hiyo kufuatia mapendekezo yaliyotolewa na Kimberly Process.

Kimberly Process ni chombo kinachoratibu biashara ya almasi duniani.

Mapema mwezi huu, jopo la Kimberly lilitoa miezi sita kwa Zimbabwe kuimarisha mazingira katika eneo linalochimbwa almasi iitwayo Marange.

Jopo hilo linaishutumu jeshi la Zimbabwe kwa mauaji na kulazimisha watu kuondoka eneo la migodi hiyo.

Waziri wa madini nchini humo Obert Mpofu ameliambia gazeti la serikali la Herald kwamba Zimbabwe imefanya mengi kuhakikisha masharti yaliyowekwa na jopo hilo yanafuatwa.

Bw Mpofu pia amesema kulikuwa hakuna tena majeshi ya usalama katika eneo hilo.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha