 |
|
| Ramani ya Ethiopia |
Waasi wa kikabila wa Kisomali kusini mashariki mwa Ethiopia wamesema wameshambulia majeshi ya serikali na kukamata miji kadhaa.
Waasi hao wa Ogaden National Liberation Front (ONLF) wamesema siku ya Jumanne walianza kushambulia mistari ya mbele ya uwanja
wa mapambano.
Wakieleza zaidi waasi hao wamesema "idadi kubwa" ya wanajeshi wa Ethiopia waliuawa na zana zao wamezikamata.
Taarifa hizo bado hazijathibitishwa na siku za nyuma Ethiopia imekuwa ikupuuza taarifa hizo za waasi kufanikiwa katika medani
ya kivita.
|