|
Obama na mikakati ya Afghanistan
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Rais wa Marekani Barack Obama amekutana na kamati yake ya usalama wa taifa kujadili mikakati ya Afghanistan, huku tetesi zikiongezeka
kuhusu uamuzi wa idadi ya wanajeshi wanaopigana huko.
Maafisa wa Ikulu ya Marekani wamesema rais Obama amejadili suala la muda na mapendekezo manne yaliyowasilishwa na washauri wake, lakini hakuna uamuzi wowote umefikiwa. Maafisa wa Ikulu wameongeza kuwa rais huyo amesema nia ya Marekani haitomalizika bila dira, na kuwa utawala bora lazima upige hatua. Waziri mkuu wa Uingereza, Gordon Brown ameliambia bunge la nchi hiyo kuwa anatarajia uamuzi kutangazwa hivi karibuni. 'Nimezungumza na Rais Obama na ninatarajia atatangaza uamuzi huo siku chache zijazo, na ni wanajeshi wangapi watahusika,' Bw Brown amewaambia wabunge. |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||