BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 11 Novemba, 2009 - Imetolewa 17:38 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Mjerumani ahukumiwa maisha jela
 
Alex Wiens alikaa nyuma ya glasi isiyopitwa na risasi akizungukwa na wanausalama wakati wa hukumu ya maisha. Itakumbukwa kua ni mwezi julayi, alipompiga kisu na kumuua Marwa el Sherbini katika mahakama hio hio.

Ujeremani ni nchi ya pili kwa kua na idadi kubwa ya Waislamu barani Ulaya na tukio hilo lilizua ghadhabu katika mataifa ya Waislamu baada ya Ujerumani kuchelewa kulaani kisa hicho.

Mamiya ya Waislamu walikusanyika nje na kusali wakiitaka serikali iwajibike zaidi dhidi ya ubaguzi. Wakati wote huo Alex Wiens ambaye ni raia wa Ujerumani, mzaliwa wa Urussi alidai kua hakukusudia. Lakini mwanasheria mkuu wa Ujerumani alisema ni bayana kwamba sababu yake kuu ni chuki kwa waislamu.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha