BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa:
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Mauaji ya mtoto yaibua hasira A.Kusini
 
Mkuu wa polisi wa Afrika Kusini amelaani ufyatuliaji risasi kwa mtoto wa kiume wa umri wa miaka mitatu yaliyofanywa na ofisa wa polisi.

Bheki Cele ameyapuuza madai ya afisa huyo kwamba alifyatua risasi kujihami akiamini bomba alilokuwa ameshika mtoto huyo ni bunduki.

Ameiambia BBC kwamba mauaji hayo ni uhalifu wa kizembe akisema: "Hata kama ingekuwa bunduki ya kweli, usingeanza kufyatua risasi."

Lakini alitetea haki ya polisi kuweza kutumia nguvu inapobidi.

Atlegang Aphane alikuwa ndani ya gari ambalo polisi walidhani linaendeshwa na wanaoshukiwa kuwa wahalifu alipopigwa risasi siku ya Jumanne.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha