|
Rais wa zamani wa Liberia, Charles Taylor, ametoa ushahidi katika Mahakama ya The Hague kuwa alidanganywa na Nigeria kabla
ya kutiwa mbaroni na kisha kushtakiwa katika mahakama hiyo ya ICC.
Taylor anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu wa kiivita katika Mahakama Maalumu ya Sierra Leone kwa kuwaaunga mkono waasi waliowafanyia
raia wa Sierra Leone ukatili mkubwa kunako miaka ya 90.
Taylor alikuwa uhamishoni nchini Nigeria mwaka 2006 alipotiwa mbaroni. Alidai kuwa kiongozi wa wakati huo wa Nigeria, Olesugun
Obasanjo, alimwambia alikuwa huru kuondoka, lakini kisha akapanga atiwe mbaroni kwa kujaribu kutoroka.
|