|
Mradi wa usafiri Afrika Kusini njia panda
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Moja ya mradi mkubwa wa miundombinu nchini Afrika Kusini, wa matayarisho ya Kombe la Dunia, mwaka ujao, hautakuwa tayari ifikapo
wakati huo.
Msemaji wa shirika la reli iendayo kwa kasi - Gautrain - ameiambia BBC kuwa reli hiyo haitaanza kazi rasmi, hadi wiki mbili baada ya michuano hiyo kuanza. Mwandishi wa BBC mjini Johannesburg, Jonah Fisher amesema taarifa hizi ni pigo kwa matarajio ya Afrika Kusini kuandaa michuano yenye mafanikio makubwa. Katika tukio lingine, waandalizi wa Kombe la dunia wamelaani kupaa kwa kodi za nyumba kwa ajili ya tukio hilo. Mkuu wa kamati ya maandalizi Danny Jordaan amesema bei kubwa zinaweza kuathiri matarajio ya Afrika Kusini ya kuwashawishi
watalii kurejea tena baada ya Kombe la Dunia. |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||