|
Meli ya mafuta yanusurika kutekwa
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Jeshi la kupambana na maharamia la Umoja wa Ulaya limesema maharamia wa kisomali wameshambulia meli ya mafuta, karibu kilomita
elfu 2 kutoka pwani ya Somalia.
Meli hiyo iliyosajiliwa Hong Kong, iliweza kukimbia shambulio hilo lililofanywa na vyombo viwili vya majini, vinendavyo kwa kasi. maharamia katika chombo hicho walikuwa wakifyatua risasi na mabomu ya roketi. Shambulio hili limeelezwa kuwa kuwa la kwanza kufanyika mbali zaidi na pwani ya Somalia. Wakati huohuo, taarifa za wataalam wa baharini zinasema maharamia wameteka meli ambayo ina shehena ya silaha. Takriban meli 40 kutoka Umoja wa Ulaya, Marekani, China, India na Japan, zinahusika na shughuli za kupambana na uzuiaji wa utekaji nyara unaofanywa na maharamia, hasa katika eneo la Ghuba ya Uajemi. |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||