|
Wamarekani watatu wanaoshikiliwa nchini Iran kwa tuhuma kuingia nchini humo kinyume cha cheria, watashitakiwa kwa makosa ya
ujasusi.
Shirika la habari la Iran, IRNA limesema wamarekani hao, Shane Bauer, sarah Shroud na Joshua Fattal, wanashikiliwa na mamlaka
za Iran tangu mwishoni mwa mwezi Julai.
Watatu hao wanadhaniwa kuvuka mpaka kimakosa, wakati wakifanya matembezi katika eneo la Wakurdi, nchini Iraq.
Akizungumza mjini Berlin, Ujerumani, waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Hilary Clinton amelaani taarifa hizo na kutoa wito
wa watu hao kuachiliwa.
|