|
Ripoti inayoeleza hali ya wafungwa nchini Eritrea, imechapishwa na kituo cha amani na haki za binadam cha mjini Oslo.
Kwa mujibu wa Ripoti hiyo kuna magereza kadhaa, mengine katika visiwa vya mbali katika Bahari ya Sham vijulikanavyo kama Dahlak
huku wengine wakiwa ndani ya ma-container.
Wafungwa huning'inizwa juu chini, na kuachwa siku kadha, kwenye jua na mvua na wengine wanapotea tu na miili huonekana mabara-barani.
Mtu yeyote anaweza kukamatwa Eritrea kwa sababu yoyote au bila ya sababu. Na kutokuwepo kwa vyombo huru vya habari, vyama
vya upinzani au waandishi wa habari wa kigeni hali inaendelea bila ya kuripotiwa.
|