|
Mahasimu nchini Madagascar waafikiana
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
Viongozi mahasimu wa kisiasa wa Madagascar wamekubaliana kuunda serikali ya pamoja baada ya mivutano ya miezi kadha.
Kiongozi wa sasa wa Madagascar Andry Rajoelina amesema viongozi wanne wamekubaliana katika mazungumzo yaliyofanyika Addis Ababa, Ethiopia, yeye aendelee kuwa Rais hadi uchaguzi ujao mwakani. Amesema badala ya kuwa na makamu wa rais, kutakuwa na marais wawili watakaoshirikiana wakiwakilisha vyama vya siasa. Bw Rajoelina alimpindua Marc Ravalomanana mwezi wa Machi, lakini ameshindwa kutambuliwa na jumuia ya kimataifa. Bw Rajoelina pamoja na washirikia wake ambao walimshutumu Ravalomanana kwa ufujaji wa fedha za umma, wenyewe wameshutumiwa na Muungano wa Afrika kwa kupindua serikali na misaada kutoka nje ikasimamishwa. Mahasimu hao wawili pamoja na marais wawili wa zamani, Didier Ratsiraka na Albert Zafy, walikubaliana mwezi wa Agosti kuwa
na kipindi cha mpito cha miezi 15, lakini hadi sasa wamekuwa wakivutana juu ya makubaliano hayo. |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||