BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 06 Novemba, 2009 - Imetolewa 18:07 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Mzinifu apigwa mawe hadi kufa Somalia
 
Wanamgambo kusini mwa Somalia, wamempiga mawe hadi kufa mwanaume mmoja aliyekiri mbele ya mahakama ya kiisilamu kuwa mzinifu.

Hata hivyo mpenzi wa mwanaume huyo alinusurika kifo kwa kuwa ni mja mzito.

Abas Hussein Abdirahman, mwenye umri wa miaka 33, aliuawa mbele ya umati wa watu takriban miatatu katika mji wa bandari wa Merka.

Afisaa mmoja wa kundi la al-Shabab amesema kuwa mwanamke huyo atauawa baada ya kujifungua mwanawe.

Makundi ya wapiganaji yanadhibiti maeneo ya kusini mwa Somalia huku serikali ya mpti ikiwa na udhibiti wa sehemu za mji mkuu Mogadishu.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha