BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 06 Novemba, 2009 - Imetolewa 01:49 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Saudia yaiondoshea vikwazo Somalia
 
Saudi Arabia imeondoa vikwazo vya kuingiza mifugo kutoka Somali vilivyowekwa miaka tisa iliyopita kuzuia kuenea kwa homa ya Rift Valley.

Baadhi ya wachungaji na wafanyabiashara wamefurahishwa na hatua hiyo.

Inamaanisha kuwa wataweza kufaidika kutokana na mifugo hiyo kuhitajika sana wakati wa sikukuu ya Eid al-Adha ambapo waislamu aghlabu huchinja mnyama.

Uuzaji wa kondoo, mbuzi na ng'ombe nje ya nchi ni uti wa mgongo wa uchumi wa Somalia na Saudi Arabia ilikuwa soko lake kuu.

Nchi ya Somalia iliyopo kwenye pembe ya Afrika haijawa na serikali thabiti tangu mwaka 1991.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha