|
Vijana wa Nigeria waichapa N.Zealand
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Timu ya vijana wenye umri ulio chini ya miaka kumi na saba inasherehekea kufuzu kwa robo fainali ya Kombe la Dunia la vijana
wenye umri huo nchini Nigeria.
Hii ni baada ya kuifunga New Zealand mabao 5 - 0 mjini Abuja jana jioni. Hadi mapumziko Nigeria ilihesabu mabao mawili ya Edafe Egbede na moja la Stanley Okoro na baada ya mapumziko Sani Emmanuel akaongezea mawili kuiona Nigeria ikibaki peke kati ya Timu za Afrika katika Kombe hili. Nigeria sasa itapambana na Korea ya kusini iliyofuzu baada ya kuinyuka Mexico kwaz matuta 5 - 3 baada ya kipindi cha dakika 90 kumalizika pande zote zikihesabu 1-1. Kabla ya Nigeria kufuzu Burkina Faso ilikuwa tayari imefungishwa virago na Uhispania iliyoichapa 4 -1 mjini Kano. |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||