 |
|
| DRC imewahi kutoa washambulizi wengi wenye sifa kama za LuaLua na bila shaka Mazembe haitakosa wachezaji kama hao |
Klabu ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ya soka, TP Mazembe, huenda ikawa bingwa wa Afrika kesho Jumamosi, baada ya miaka
41, ikiwa itaishinda Heartland kutoka Nigeria mjini Lubumbashi.
TP Mazembe ilishindwa magoli 2-1 katika mechi ya mkondo wa kwanza Nigeria.
Hakuna hata mchezaji mmoja wa Congo alikuwa amezaliwa wakati timu ya Congo ya 'Crows', yaani Kunguru, ilipoishinda Etoile
Filante ya Togo jumla ya magoli 6-4 na kulihifadhi kombe hilo miaka 41 iliyopita.
Timu hiyo iliyoanzishwa na watawa wa Benedict miaka 70 iliyopita, na ikijulikana kama TP Englebert, iliandikisha historia
kwa kuwa timu ya kwanza kufanikiwa kulihifadhi kombe.
Rekodi ilidumu kwa miaka mingi, hadi Enyimba ya Nigeria ilipofanikiwa kulihifadhi kombe hilo mwaka 2004.
|