BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 06 Novemba, 2009 - Imetolewa 03:23 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Eneo la maziwa makuu lasaidiwa
 
Mkutano wa kimataifa wa waihsani unaofanyika nchini Burundi unatarajia kukusanya zaidi ya dola za kimarekani bilioni moja.

Fedha hizo ni kwa ajili ya kufadhili miradi ya kimaendeleo katika eneo la maziwa makuu barani Afrika.

Mmoja wa waandaaji wa mkutano huo, Liberata Mulamula, amesema nchi waihsani wanatakiwa kuhakikisha kuwa eneo hilo lina amani na usalama thabit.

Amesema hatua hiyo ni muhimu kuetekelezwa kama ilivyoahidiwa katika mkataba ujulikanao kama Makubaliano ya Nairobi.

Makubaliano hayo yalitiwa saini na nchi 11 za Afrika zilizokumbwa na migogoro.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha