BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 05 Novemba, 2009 - Imetolewa 05:23 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Mgogoro wa Zimbabwe wajadiliwa
 
Wapatanishi wa kusini mwa Afrika wanatarajia kuanza mazungumzo nchini Msumbiji kwa nia ya kuzuia kuporomoka kwa serikali ya muungano ya Zimbabwe.

Serikali hiyo imekuwa na mgogoro tangu waziri mkuu Morgan Tsvangirai alipoanza kugomea vikao vya bunge.

Bw Tsvangirai anapinga namna rais Robert Mugabe anavyotekeleza mpango wa kugawana madaraka.

Serikali ya Zimbabwe pia ipo katika uangalizi kwenye mkutano wa kimataifa nchini Namibia unaohusu usimamizi wa mauzo ya almasi.

Mkutano huo unajadili aidha kuitoa Zimbabwe katika mpango huo kufuatia madai kwamba polisi na jeshi walihusika kuvunja haki za binadamu kwenye mgodi wa almasi wa Marange, penye utajiri mkubwa wa madini hayo duniani.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha