BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 05 Novemba, 2009 - Imetolewa 12:14 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
ICC kuanzisha uchunguzi Kenya
 
Ni rasmi sasa Mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC itawafungulia mashtaka washukiwa wakuu wa machafuko ya baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2007 nchini Kenya.

Mwendesha mashtaka mkuu wa mahakama hiyo aliye nchini Kenya Louis Moreno-Ocampo amesema kuwa ataanzisha uchunguzi dhidi ya washukiwa wakuu wa machafuko hayo mwezi Ujao.

Ocampo ameyasema haya aliopohutubia waandishi wa habari muda mfupi baada ya kufanya mkutano wa faragha na rais Mwai Kibaki na waziri mkuu wa Kenya Raila Odinga mjini Nairobi.

Kwa Upande wake Kenya imesema kuwa itashirikiana na mahakama hiyo ya ICC.Waziri mkuu Raila Odinga amesema kuwa serikali itafanya hivyo ili kuhakikisha kuwa yale yaliyotokea baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2007 hayatokei tena.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha