|
Moreno-Ocampo azungumza nchini Kenya
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Mwendesha mashitaka mkuu wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita, ICC, Luis Moreno-Ocampo, anatarajiwa kufanya mazungumzo
nchini Kenya siku ya Alhamis.
Mazungumzo hayo ni namna ya kuhakikisha haki inatendeka kwa wale wanoshukiwa kuhusika na ghasia zilizotokea baada ya uchaguzi mwaka 2008. Bw Moreno-Ocampo amesema kama serikali ya Kenya itashindwa kuchukua hatua zozote, basi yeye mwenyewe atashinikiza hatua zichukuliwe. Zaidi ya watu elfu moja waliuawa katika ghasia hizo. Uchunguzi wa serikali ya Kenya mapema mwaka huu ulipendekeza suala hilo kupelekwa katika mahakama hiyo ya ICC, the Hague lakini
inaweza isfikishwe iwapo mahakama maalum itaundwa nchini humo. |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||