|
Kamanda mmoja mkuu wa kundi la waasi la LRA nchini Uganda, amejisalimisha kwa jeshi la nchi hiyo.
Charles Arop alikuwa mmoja wa makamanda wa kundi hilo aliyetuhumiwa kuongoza mauaji ya halaiki wakati wa krimasmasi kaskazini
mashariki mwa Congo ambapo watu miamoja arobaini na tatu raia wa Congo waliuawa.
Msemaji wa jeshi la Uganda Meja Felix Kulayigye akiongea na BBC amesema tayari kamanda huyo amepelekwa katika mji wa Gulu
Uganda.
Inaarifiwa kamanda Arop alijisalimisha siku ya jumanne kwa wanajeshi wa Uganda wanaoshika doria kaskazini mashariki kwa Jamuhuri
ya kidemokrasia ya Congo.
|