 |
|
| Timu ya Ferrari ilishindwa kuwika katika mashindano ya msimu 2009 |
Timu ya Ferrari imetangaza kwamba waliopewa jukumu la kusimamia mashindano ya magari ya Formula 1 wamekuwa wakiyapiga vita
makampuni makubwa ya kuunda magari, na timu kadha kulazimika kujiondoa katika mashindano hayo.
Toyota ilitangaza siku ya Jumatano uamuzi wa kujiondoa katika mashindano hayo.
Hayo ni baada ya kuondoka kwa Honda na BMW, huku Renault ikisema bado inafikiria kama itaendelea kuwepo katika mashindano
au la.
Taarifa ya Ferrari imeelezea maoni hayo mara tu baada ya mabadiliko katika baraza linalosimamia mashindano ya magari, FIA.
Madaraka ya rais Max Mosley sasa yamechukuliwa na aliyekuwa mkuu wa Ferrari hapo zamani, Jean Todt.
|