BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 04 Novemba, 2009 - Imetolewa 17:29 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Mwanasheria mkuu Kenya akiri Marufuku
 
Mkuu wa Sheria nchini Kenya Amos Wako Amethibitisha kuwa yeye ndiye afisa wa ngazi ya juu aliyepigwa marufuku kuzuru Marekani.

Amos Wako amesema kuwa amepokea barua kutoka kwa ubalozi wa marekani na ni miongoni mwa maafisa wengine kumi na watano wa ngazi ya juu serikalini walioandikiwa barua ya kufuta hati zao za usafiri kuzuru nchi hiyo.

Jumatatu wiki iliyopita, naibu wa waziri wa kigeni wa Marekani wa masuala ya Afrika Johnie Carson alitangaza kuwa Marekani imewapiga marufuku maafisa kumi na watano wa ngazi za juu katika serikali ya Kenya kwa kuwa kizuizi kikubwa katika mabadiliko ya sheria nchini humo.

Akihutubia kwenye televisheni ya Kitaifa muda mfupi uliopita, Wako alikanusha madai kuwa amehusika kuvuruga marekebisho nchini , akisema kuwa amekuwa mstari wa mbele kupigania marekebisho hayo.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha