BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 03 Novemba, 2009 - Imetolewa 01:56 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Theluji yayeuka mlima Kilimanjaro Tanzania
 
Wanasayansi kutoka Marekani wamegundua kuwa theluji na barafu katika mlima mrefu barani Afrika, Kilimanjaro uliopo nchini Tanzania inayeyuka kwa kasi na huenda ikatoweka ndani ya miaka 20.

Utafiti huo ambao umechapishwa katika jarida la Proceedings of the National Academy of Sciences, ulikuwa wa kwanza kujua kiwango cha barafu kilichopotea katika mlima huo.

Umegundua kuwa tandiko kuu la barafu hiyo lilisinyaa kwa asilimia themanini na tano tangu mwaka 1912.

Barafu nyingine ilisinyaa kwa zaidi ya asilimia hamsini katika kipindi cha miaka tisa iliyopita.

Utafiti huo umebaini kuongezeka kwa joto la dunia huenda ikawa ndio sababu ya kuyeyuka kwa theluji hiyo.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha