BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 03 Novemba, 2009 - Imetolewa 00:31 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Mpambanaji wa ufisadi auawa Liberia
 
Watu wenye silaha nchini Liberia wamemwuua afisa mmoja aliyekuwa akihusika na kupambana na ufisadi hasa katika mikataba ya umma.

Keith Juba alipigwa risasi mfululizo siku ya Jumapili usiku nje ya nyumba yake, ambapo ni kilomita 60 kutoka mji mkuu wa Monrovia.

Hadi sasa polisi hawajasema iwapo mauaji hayo yana uhusiano na nafasi aliyokuwa nayo Bw Jubah ya mkuu wa tume inayoshughulikia mikataba ya umma.

Tume hiyo huhakikisha kuwa mikataba hasa ile mikubwa inayohusu migodi ni halali.

Mmoja wa ndugu zake Bw Jubah ambaye hakutaka jina lake litajwe ameiambia BBC kuwa mwili wake uliwaka moto.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha