|
E Guinea yamsamehe Mann
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Mwanajeshi wa zamani wa uingereza Simon Mann, aliyehukumiwa kifungo cha miaka 34 kwa kupanga mapinduzi nchini Equatorial Guinea,amepewa
msamaha,serikali imesema.
Mshauri wa rais, Miguel Mifuno,ameiambia BBC kuwa Mann alilazimika kuondoka nchini katika muda wa saa 24. Wizara ya mambo ya nje ya uingereza imesema inafahamu kuwa kuachiliwa huru kwa Mann ni uamuzi binafsi wa rais kwa misingi ya kibinadamu. Mann, aliyehukumiwa kifungo mwezi Julai mwaka 2008, alikiri kula njama ya kumpindua rais Teodoro Obiang Nguema wakati wa kesi yake. Bwana Mifuno amesema Mann aliachiliwa huru kwa misingi ya kibinadamu kuhusiana na afya yake. |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||