BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 02 Novemba, 2009 - Imetolewa 12:04 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Biashara ya almasi zimbabwe ikomeshwe
 
Zimbabwe inakabiliwa na shinikizo kutoka kwa jamii ya kimataifa ifurushwe kutoka kwenye biashara ya kimataifa ya almasi kufuatia madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu dhidi ya wanajeshi wake.

Halmashauri ya kimataifa inayosimamia biashara hiyo, 'Kimberly Process' imetakiwa na wanaharakati wa haki za kibinadamu kukomesha Zimbabwe kuuza almasi.

Kilio hiki kimejitokeza kufuatia tuhuma dhidi ya wanajeshi wa nchi hiyo kuwatesa raia. Kwa mujibu wa wakereketwa wa haki za binadamu, wanajeshi wamewaua takriban watu miambili katika migodi ya almasi, ingawa serikali imekanusha madai hayo.

Halmashauri hiyo yenye wanachama sabini, iliundwa mwaka wa 2003, kwa minajili ya kuwahakikishia wateja wa bidhaa hiyo kwamba Almasi wanayonunua haitumiki kufadhili vita au ukiukwaji wa haki za binadamu.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha