|
Jaji wa mahakama kuu ya Tanzania, amewahukumu kunyongwa watu wanne waliopatikana na hatia ya mauaji ya mlemavu wa ngozi yaani
albino mwaka uliopita.
Mwandishi wa BBC huko magharibi mwa Tanzania, aliyekuwepo mahakamani wakati hukumu hiyo ikitolewa, amesema watu hao wamebainika
na hatia ya kufanya mauaji hayo katika wilaya ya Bariadi mwishoni mwa mwaka jana.
Hii ni hukumu ya pili ya kifo kutolewa katika kipindi cha takriban mwezi mmoja dhidi ya watuhumiwa wa vitendo vya mauaji ya
albino ambayo yalianza kujitokeza miaka miwili iliyopita nchini humo.
|