|
UN yajitenga na jeshi la Congo
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Umoja wa mataifa umesitisha kuunga mkono kitengo cha jeshi la jamhuri ya kidemokrasi ya Congo,ikishutumu wanajeshi kwa mauaji
ya watu 62,afisa mmoja mkuu wa umoja wa mataifa amesema.
Mkuu wa vikosi vya kulinda amani wa umoja wa mataifa Alain Le Roy amesema kuwa ana taarifa kwamba jeshi ''lililenga kwa maksudi'' raia. Watetezi wa haki za binaadamu wamesisitiza kuwa watu wa kabila la wahutu wamekuwa wakiuawa na wanajeshi wa Congo, na wamelaumu umoja wa mataifa kwa kutojitahidi kuzuia mauaji hayo. Umoja wa mataifa umekuwa ukisaidia jeshi kukabiliana na waasi wa kihutu wa Rwanda tangu mwezi Januari. Kufwatia ziara ya eneo hilo, bwana Le Roy alisema jeshi limewaua raia 62 kati ya mwezi mei na septemba mwaka huu. |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||