|
Kanisa la kilutheri nchini Sweden lenye waumini wengi zaidi nchini humo limekubali kubariki ndoa za wapenzi wa jinsia moja
kuanzia mwezi ujao.
Asilimia 70 ya baraza kuu la kanisa hilo lilipigia kura kuunga mkono hatua hiyo. Kanisa la kilutheri limejiunga na imani nyingine
chache duniani zinazokubaliana na ndoa za wapenzi wa jinsia moja.
Serikali ya Sweden imepitisha sheria mpya kulinda wapenzi wa jinsia moja. Robo tatu ya raia wa Sweden ni waumini wa Lutheran,
japo idadi ya wanaohudhuria ibada imepungua sana.
|