BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 02 Januari, 2008 - Imetolewa 15:01 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Diplomasia yaingilia kati ghasia za Kenya
 

 
 
David Miliband, waziri wa mambo ya nje wa Uingereza.
Nchi wahisani zinajaribu zaidi kutumia diplomasia kutuliza ghasia badala ya vikwazo.

Pande zote mbili katika mzozo wa uchaguzi wa Kenya zimetupiana lawama za kuchochea ghasia huku jitihada za kidiplomasia zikifanyika kutuliza mgogoro wa kisiasa nchini humo.

Watu wasiopungua 275 wameuawa, wakiwemo 30 magharibi mwa Kenya ambao walichomwa moto ndani ya kanisa walikoenda kuomba hifadhi.

Idadi kubwa ya wananchi wamekuwa wakiomba hifadhi katika maeneo salama kuepuka magenge ya watu wenye silaha na waporaji mali huku wasi wasi ukizidi wa mashambulio zaidi na kulipizana visasi.

Polisi katika mji mkuu Nairobi wameweka vizuizi vya barabarani kwenye maeneo muhimu ya kuingilia katikati ya jiji na kudhibiti mwenendo wa magari.

Pamoja na hali kuonekana kuanza kuwa tulivu, bado kuna wasi wasi kwamba ghasia zinaweza kuzuka upya endapo mkutano wa wapinzani ulioitishwa kesho utafanyika.

 
 
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha