BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 15 Julai, 2009 - Imetolewa 01:26 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Pembe haramu zanaswa nchini Kenya
 

 
 
Maafisa wa KWS wakionyesha pembe hizo
Kifaru mweusi hupatikana tu mashariki na kusini mwa Afrika

Maafisa wa huduma za wanyama wa pori nchini Kenya, KWS, wamenasa pembe za ndovu na vifaru weusi zikiwa zimefichwa katika jeneza lililokuwa likisafirishwa kwa ndege hadi Laos.

Thamani ya pembe hizo 16 inakadiriwa kuwa dola za Marekani milioni moja.

Kwa mujibu wa maafisa hao, damu iliyopatikana kwa pembe hizo zenye uzani wa kilogramu 300 zilinyofolewa kutoka kwa tembo na vifaru hivi majuzi.

Ndege hiyo ilikuwa imetoka Msumbiji na kutua mjini Nairobi ikiwa safarini kuelekea nchini Thailand na hatimaye Laos.

Asili ya pembe hizo haijulikani ingawa maafisa wa KWS wanasema kwamba huenda zilitolewa nchini Tanzania au Afrika Kusini.

Kifaru mweusi ni mnyama adimu sana na hupatikana tu katika maeneo ya mashariki na kusini mwa Afrika.

Biashara ya pembe za ndovu na wanyama kama vile kifaru mweusi ambao idadi yao inaendelea kudidimia, ilipigwa marufuku mnamo mwaka wa 1989.

Lakini baadhi ya nchi hazitekelezi marufuku hiyo.

 
 
VIUNGO VYA MTANDAO WA HAPA HAPA
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha