BBCSwahili.com
Maziwa Makuu
Kisomali
Arabik
Kifaransa kwa Afrika
Turqisht
 
Mara ya mwisho imebadilishwa: 11 Julai, 2009 - Imetolewa 17:19 GMT
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
Obama awashauri Waafrika
 

 
 
Ni ziara ya kwanza ya Rais Obama kusini mwa jangwa la Sahara
Rais Obama ameshauri Afrika iwajibike na mstakabali wake
Rais Barack Obama akiwa katika ziara yake ya kwanza kusini mwa jangwa la Sahara amesema bara la Afrika lazima liwajibike kuhusiana na mstakabali wake katika ulimwengu.

Bwana Obama pia ameambia bunge la Ghana kwamba utawala bora ni muhimu sana kwa maendeleo.

Amesema Afrika inakabiliwa na changamoto nyingi sana, lakini akaongeza kuwa Marekani italisaidia bara hilo.

Ikiwa ilichaguliwa kwa ajili ya ziara ya Rais Obama kwa kuwa ni mfano bora wa demokrasia barani Afrika.

Rais huyo wa Marekani amesema enzi ya ukoloni ilikuza mizozo katika bara la Afrika, lakini akaongeza kuwa nchi za magharibi sio za kulaumiwa kwa kuporomoka kwa uchumi wa Zimbabwe , kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoshirikisha watoto sehemu mbali mbali barani Afrika.

Alisifu ufanisi wa Ghana wa utawala bora na ukuaji wa uchumi , akisema ingawa hatua hiyo haijakuwa ya kusisimua kama vita vya kuikomboa Ghana kutoka utawala wa ukoloni, lakini ni muhimu sana.

Hotuba ya Rais Obama kwa Afrika imezingatia maeneo manne muhimu kwa Afrika : demokrasia, fursa za kujiendeleza , afya na kusuluhisha mizozo kwa amani.

Rais Obama alizungumzia mwanzo mpya kwa kwa bara la Afrika.

Alisema mstakabali wa bara hilo una Waafrika wenyewe .

Barack Obama aligusia ndoto za viongozi wa Afrika waliopigania Uhuru , ambazo mara nyingi hazikutimia , lakini akaelezea matumaini yake kwamba hali sasa inabadilika katika bara hilo.

Aliisifu Ghana kwa ufanisi wake katika utawala wa kidemokrasia, lakini akasisitiza kuwa kinachofanyika kati ya uchaguzi mmoja na ule mwingine ni muhimu sana.

Ametoa wito wa kumalizika kwa ufisadi na utawala wa kidhalimu.

Rais Obama amesema bara la Afrika halihitaji watu wenye nguvu, badala yake linahitaji taasisi zilizoimarika.

Alisema ni jukumu la kizazi cha vijana kuwawajibisha viongozi.

 
 
VIUNGO VYA MTANDAO WA HAPA HAPA
Maharamia wateka meli ya Marekani
10 Aprili, 2009 | Vivutio
HABARI MPYA
 
 
Mtumie rafiki barua pepe   Chapisha
 
  Idhaa Yetu | Wasiliana Nasi
 
BBC Copyright Logo ^^ Rejea Juu
 
  Habari | Hali Ya Hewa
 
  BBC News >> | BBC Sport >> | BBC Weather >> | BBC World Service >> | BBC Languages >>
 
  Msaada | Wasiliana nasi | Maelezo ya Faragha