bbc.co.uk navigation

Terry Connor sasa meneja wa Wolves

Imebadilishwa: 24 Februari, 2012 - Saa 10:51 GMT
Mick McCarthy

McCarthy alitimuliwa baada ya Wolves kufunga magoli 5-1 na West Brom katika uwanja wa nyumbani

Klabu ya Wolves imempandisha cheo meneja msaidizi wa Wolves.

Terry Connor sasa atashikilia madaraka hayo ya meneja hadi mwisho wa msimu.

Klabu kilimfuta kazi Mick McCarthy tarehe 13 Februari mara tu baada ya kushindwa magoli 5-1 na mahasimu wao West Brom.

Wolves wameamua kumpandisha cheo Connor baada ya Walter Smith, Alan Curbishley na Brain McDermott kuamua hawaitaki kazi hiyo ya kuiongoza Wolves.

"Hii ni hatua muwafaka ambayo ina msimamo halisi. Wachezaji wanaiunga mkono kikamilifu", ameelezea tajiri anayemiliki klabu ya Wolves, Steve Morgan.

"Tangu tulipofanya uamuzi kwa shida kuachana na Mick, tumepitia utaratibu kwa makini katika kumchagua mtu atakayefaa.

"Baada ya kushauriana na watu kadha katika utaratibu huu, mimi na bodi tumeamua kwa pamoja Terry ndiye mtu atakayefaa kukiongoza klabu hadi mwisho wa msimu".

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.