bbc.co.uk navigation

Mancini abeba lawama kufungwa na Everton

Imebadilishwa: 1 Februari, 2012 - Saa 11:40 GMT

Meneja wa Manchester City Roberto Mancini amesema anawajibika kwa kutoiandaa vyema timu yake baada ya kuteleza na kufungwa bao 1-0 na Everton.

Roberto Mancini ajilaumu kwa kutoiandaa timu dhidi ya Everton

Roberto Mancini ajilaumu kwa kutoiandaa timu dhidi ya Everton

Vinara hao wa Ligi Kuu ya England kwa sasa, bado wanaendelea kushikilia usukani wa ligi hiyo kwa tofauti ya mabao baada ya Darron Gibson kupachika bao hilo moja, wakati Manchester United waliichabanga Stoke katika uwanja wa Old Trafford.

"Huenda yalikuwa ni makosa yangu kwa sababu hatukujiandaa vizuri kwa mechi hii," Mancini aliiambia BBC.

"Nilifikiria kabla ya mchezo kwamba mambo yangekuwa rahisi, kumbe yakawa kinyume."

Mancini baadae alikiri alifanya makosa wakati wa kuiandaa timu.

"Wachezaji wangu walijituma sana uwanjani lakini nilifanya baadhi ya makosa siku tatu zilizopita kwa kuiandaa mechi hii," aliongeza.

Kiungo wa zamani wa Manchester United, Gibson alipachika bao hilo pekee kipindi cha pili na kuipa timu yake ya zamani nafasi nzuri ya kuisogelea Manchester City, wakati mabingwa hao wa Ligi ya England walipoilaza Stoke mabao 2-0 na kuziba pengo la pointi.

Mancini alikiri timu yake ilikuwa na kibarua kigumu dhidi ya timu ambayo imewahi kuifunga mara moja tu katika michezo 14 katika uwanja wa Goodison Park.

"Everton wakiwa kwao ni wazuru sana," aliongeza. "Kila wakati tunapocheza nao wanacheza vizuri sana.

Taarifa zinazohusiana

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.