Khan kuzichapa tena na Lamont

Imebadilishwa: 13 Januari, 2012 - Saa 12:17 GMT
Peterson

Peterson atalazimika kupanda tena ulingoni

Mpambano kati ya Amir Khan na Lamont Peterson umethibitishwa na Chama cha Ngumi cha Dunia, WBA, kwa mujibu wa promota wa Khan.

Richard Schaefer amesema amepokea barua kutoka kwa WBA ikimjulisha kuhusu "uamuzi wao rasmi wa kuwepo na mpambano wa marudio mapema iwezekanavyo."

Khan alipoteza mikanda yake ya WBA na IBF kwa Peterson mwezi Disemba na alihoji vigezo kadhaa vilivyotumika katika mpambano huo.

Lakini Peterson anaweza kuuacha mkanda wa WBA kwa kuamua kutopigana.

Schaefer, ambaye ni mkurugenzi mkuu wa kampuni ya Golden Boys ya promosheni alikiambia kituo cha michezo cha ESPN: "Nimefurahi amepata mpambano wa marudiano, nina imani tutaanza majadiliano na kufanikisha pambano hilo.

"Amir na Lamont ni vijana wazuri na wanamichezo mahiri ambao walipigana kwa dhati mjini Washington mwezi Disemba, na nina uhakika uamuzi huu utafirahiwa na mashabiki wa ndondi duniani kote."

Taarifa zinazohusiana

bbc.co.uk navigation

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.