bbc.co.uk navigation

Kupambana na Saratani

Imebadilishwa: 3 Februari, 2012 - Saa 13:07 GMT

Kupambana na Saratani

  • Simon James, Uingereza
    Simon James, Uingereza: "Mwaka 2006 nilikutwa na Saratani ya utumbo na kufanyiwa upasuaji mara adhaa pamoja na tiba ya mionzi. Hii picha inanionesha mimi na kipimo cha CT miaka mitatu baada ya tiba. Sasa i miaka sita tangu nilipofanyiwa vipimo vya awali na sina saratani!"
  • Kathy, picha hii imepigwa na Jeanette Verster, Marekani.
    Kathy ana umri wa miaka 58 aliyewahi kuugua saratani ya matiti, na anaishi Cape Town, Afrika Kusini. Bado anaendelea kupatiwa matibabu ili kuhakikisha saratani hairejei tena. Picha hii ilipigwa mwaka jana baada ya kupatiwa taarifa kuwa sasa hana tena saratani. Kathy ni mtu shupavu. Nguvu yake aliipata zaidi kutokana na kuungwa mkono na mume wake, Ian na watoto wake watatu pamoja na familia yake. Picha hii imepigwa na Jeanette Verster, Marekani.
  • Zanda,  picha imepigwa na Anna Jurkovska, Latvia.
    Zanda ni mshiriki mkubwa wa "Mti wa Maisha" ambao ni mradi maalum kwa ajili ya wagonjwa wa saratani. Akiwa mama wa watoto wawili, alifanyiwa upasuaji wa saratani ya matiti na upasuaji zaidi kupunguza hatari ya saratani kurejea. Picha imepigwa na Anna Jurkovska, Latvia.
  • Zain. Picha imepigwa na Abduljalil Al-Nasser, Saudi Arabia.
    Zain aliwahi kuugua saratani. Anavaa riboni ya waridi na ni mwanaharakati hai wa kundi la The Hope. Wanachama wake hupita katika nyumba kuwatazama wagonjwa wa saratani, hasa wale ambao ndio kwanza wamekutwa na ugonjwa huo, kwa kuwa wanapitia wakati mgumu kipindi cha mwanzo. Wanazungumza waliyoyapitia, jinsi ya kupambana na tiba ya kemo na jinsi ya kutokata tamaa. Hawaachi kuwatembelea hata baada ya kupona, wanaendelea kuwatembelea wagonjwa na kuanzisha uhusiano wa karibu kabisa. Kundi la Hope (Matumaini) linapata msaada kutoka kwa watu wa kawaida hospitalini na pia Wakfu wa Saratani wa Saudi. Picha imepigwa na Abduljalil Al-Nasser, Saudi Arabia.
  • Abdullah Dhaim. Picha na Abduljalil Al-Nasser, Saudi Arabia.
    Abdullah Dhaim ana umri wa miaka 75, na alikutwa na saratani ya utumbo miaka kadhaa iliyopita. Madaktari waliondoa kipande cha sentimita 17 cha utumbo wake.Ana matumaini makubwa na baada ya kupona alianza kutembelea wagonjwa wengine wa saratani ili kuwaelimisha na kuwapa ari. Mke wake amekutwa na saratani ya ini hivi karibuni..... Wanawake wengi wanasema mara tu wanapokutwa na saratani, baadhi ya watu wanaacha hata kuwasalimia, kula nao pamoja na kuwa karibu yao. Baadhi ya watu nchini Saudi Arabia wanaamini saratani inaambukiza, au wanakuwa wanaogopa tu. Picha na Abduljalil Al-Nasser, Saudi Arabia.
  • Matt Edwards: "Huyu ni shangazi yangu Darlene Graczyk wa Bloomington, IL, Marekani. Darlene alikuwa na saratani za aina mbili za matiti. Baada ya kufanyiwa tiba ya masectomy mara mbili, kemo na mionzi, alionekana hana saratani. Ni shupavu sana. Sote tunakupenda sana".
  • Picha na Dmitry Berku, Urusi
    Dmitry Berku, Urusi: Nilikutana na Serge (kulia) miaka miwili iliyopita wakati akifanyiwa matibabu ya saratani ya damu. Alizaliwa Siberia ya Kati. Serge ana kaka na dada kadhaa na mama yake hakuwa na uwezo wa kukaa naye hospitali. Alichukuliwa na familia nyingine na hatimaye alitoka hospitali.
  • Cathleen Daum, Marekani
    Cathleen Daum, Marekani: "Mimi ni Cathy, niliwahi kuugua saratani ya matiti. Miaka 9 sasa imepita. Kuna uhusiano mzito kati yetu sote na hakuna anayeweza kuuvunja uhusiano huo...."
  • Margarita Bakhmanova, picha na Valery Klamm, Urusi.
    Margarita Bakhmanova ana umri wa miaka 37, na alikutwa na saratani miaka mitatu iliyopita. Alikuwa akisubiri matibabu ya kemo na upasuaji pia. Siku moja Margarita alikwenda kumuona rafiki yake na kumuomba ampige picha kabla hajapoteza nywele zake zote. Picha na Valery Klamm, Urusi.
  • Raphael Nzioka, Nairobi, Kenya.
    Raphael Nzioka kutoka Nairobi, Kenya, ana umri wa miaka 27 na anaugua saratani ya utumbo.
  • Kathy Rymes (kushoto) na Michelle White-Malcolm (kulia)
    Kathy Rymes (kushoto) alikutwa na saratani ya matiti mwaka 2009. Anawapa matumaini wote wenye saratani kukumbuka kuwa hawako peke yao, na kuwa kutafuta mtu wa kuzungumza naye ni muhimu wakati wa kupona. Michelle White-Malcolm (kulia) alikutwa na saratani ya matiti mwaka huo huo. Michelle anasema kuwa wagonjwa waseme jinsi wanavojisikia hasa hali ya wasiwasi ili wapatiwe msaada na watu wengine. Picha hizi zilipigwa na Scott Hussey, wa Marekani, kama sehemu ya kitabu kiitwacho Living Through Cancer (Kuishi na saratani).
  • Picha imepigwa na Eric Bowers, Marekani.
    Sanamu katika eneo la wazi la Watu waliopambana na Saratani mjini Kansas, Missouri. Picha imepigwa na Eric Bowers, Marekani. Tunawashukuru washiriki wote kwa kututumia picha zao na kuzungumzia maisha yao kwa wasomaji wetu, katika kuadhimisha Siku ya Saratani Duniani, Februari 4.

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.