|
Ukame waiathiri Kenya
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Hivi karibuni mwandishi wetu Bashkas Jugsoday alizuru sehemu kadhaa za mkoa wa Kakazini Mashariki nchini Kenya ambako ukame
umeathiri kwa kiasi kikubwa maisha ya wakazi na mifugo yako. Haya ndiyo uliyoshuhudia katika safari yake.....
Mifugo ya kila aina inaangamia kutokana na ukosefu wa maji na chakula...ni ukame mkali.
Mfugaji akimvuta ng'ombe ambaye uhai wake umekatizwa na ukame, kwa nyuma unaweza kuona mbuzi kadhaa wamekufa.
Punda yu hoi bin taaban, kazi ngumu na ukame vinakwaza maisha yake. Mkazi huyu anajaribu kumsaidia punda wake kusimama.
Ngamia, wanyama wanaojulikana kwa ustahimilivu wao jangwani, ndiyo tegemeo kwa baadhi ya wakazi kuchota maji.
Wanyama na binadamu wanagombea maji, hili ni eneo la kunyweshea wanyama kando na sehemu ya kuchotea maji kwa matumizi ya binadamu.
Wenye uwezo husubiri maji majumbani ambako gari kama hili huyafikisha na kuwauzia.
Visima vya kila aina vimechimbwa, mkazi huyo akikwangua maji kutoka kisimani, japo si mengi yanapatikana. |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||