|
Mshindi wa Faidika na BBC
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Safari ndefu ya kumtafuta kijana mwenye kipaji cha ujasiriamali ilikamilika Mombasa mwezi Agosti wakati mwenyeji Jane Mweni
alipotwaa taji la Faidika na BBC 2009, huu ni muhtasari katika picha mambo yalivyokuwa......
Mshindi wa Faidika na BBC 2009 Bi Jane Mweni, kutoka Kenya, akitabasamu na kukumbatia tuzo yake baada ya matokeo kutangazwa, Mombasa tarehe 13 Agosti 2009.
Mshindi wa tatu Bi Nyota Anjelique kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, akimpongeza Bi Mweni kwa kunyakua nafasi ya kwanza. Walioketi ni vijana wengine wanne walioingia fainali.
Mgeni rasmi wa Faidika na BBC 2009, Bi Nelly Munala kutoka Jumuiya ya Madola akisomba hotuba ya ufunguzi huku akisaidiwa na Solomon Mugera mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC.
Mkuu wa Idhaa ya Kiswahili Bw Solomon Mugera akizungumza na mshindi wa Faidika na BBC 2009, Bi Jane Mweni kwenye matangazo ya BBC baada ya ushindi wake.
Hapa hanipokonyi mtu, hii tuzo ni yangu mimi mshindi wa Faidika na BBC 2009. Bi Mweni na ushahidi wa ushindi wake...... |
VIUNGO VYA MTANDAO WA HAPA HAPA
Picha za Faidika13 Agosti, 2009 | Vivutio
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||