|
Maoni: Michael Jackson
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Yafuatayo ni baadhi ya maoni yaliyotumwa na watu mbali mbali kuhusu kifo cha mwanamuziki Michael Jackson, aliyeaga dunia akiwa
na umri wa miaka 50.
Namuombea kila la kheri huko anakokwenda pumzika kwa mengi aliyofanya hapa dunia. Nilisikitishwa kusikia habari yake ya kifo
chake jana usiku wa saa tano saa za hapa UK. Mola amuweke mahali pema nimecheza muziki wake enzi bad na mingine mingi na kuvaa
jeans zake xmas and edd-fitr.
Tutamkumbuka kwa msaada mkubwa aliutoa yeye na wanamuziki wenzake. Waliimba wimbo wa we are the world, we are the one, pesa
ziliisha wenye njaa kule Ethiopia. Huo ni mchango mkubwa sana. Ni fundisho kwa wanamuziki wote. Michael atakumbukwa kwa mengi hususani moyo wake wa kupenda watoto, ila aliniudhi alipokuwa anaukana Uafrika wake, nawasihi
wasanii wengine waige mazuri wala si mabaya kama kujibadili n.k. Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi. Amina. Michael Jackson, alikuwa mwafrika aliyeuasi Uafrika. Kitendo cha kuikana rangi na haiba yake ya Kiafrika, hakika ilikuwa ni dharau kubwa sana kwa watu wote weusi duniani. Wazungu walimpenda kwa sababu alijitahidi kuonekana kama wao. Mwisho wa siku akashindwa. Tunaweza kusema mengi kuhusu kifo chake, lakini kilicho wazi ni kwamba kemikali alizotumia kuukana Uafrika wake, zimegharimu. Hili ni somo kwa wengine wa aina hiyo, hasa ndugu zetu wa Afrika ya Kati ambao wanaona kuimba wakiwa na sura na rangi ya kiafrika, ni makosa!!! Michael amefariki. Ni jambo la kusikitisha. nitamkumbuka si kwa nyimbo na majonjo yake jukwaani, bali kwa kuwa muasi halisi
wa asili yake. Tukumbuke kuwa hakuna binadamu anayeweza kumhariri Mungu!!! Kwakweli tutabaki tunamkumbuka daima milele, Michael Jackson isitoshe yeye mwenyewe alitabiri mapema kifo chake isikuchanganye
sana kwasababu kifo kipo nakitaendelea kuwepo kwasababu sisi sote niwasafiri tumekujakutembeya apa duniani tupo njiani kuelekea
uko unakoenda, tumuombe yetu mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu maalipema peponi, Amena. Hakika ulimwengu umempoteza mtu muhimu sana namkumbuka katika staili yake ya uchezaji na uimbaji hakika pengo lake halita
zibika. Hatutakusahau milele daima. Miaka ya themanini (1980's) kulikuwa na mavazi ya (Jacksons 5 cadet) na haswa watoto ndiyo walizipenda sana. Kama wazazi hawajanunua
hizo nguo kwa ajili ya krismasi, basi nyumbani hapakaliki. Zilikuwa zinagharimu shillingi 5000 za kitanzania. Namtakia kila la heri anapokwenda. Michael alikuwa mwanamuziki hodari sana naitakia familia yake faraja kubwa sana kipindi hiki kigumu kwao. Nawashukuru pole wapenzi wa popo kwa msiba wa Jackson. Hakika hakuna atakayebakia duniani, Michael Jackson unatangulia tu. Mungu akulaze pema. Nilishtuka kidogo niliposikia taarifa juu ya kifo cha Michael Jackson. Nitamkumbuka sana katika juhudi zake za kuchangia watu
mbalimbali wanaoteseka hapa Afrika kwa kutumia kipaji chake cha muziki,mfano wimbo wa Heal the World na US For Africa, ziliweza kuchangisha fedha kwa ajili ya Africa. Mungu aitie moyo familia yake hasa kipindi hiki kigumu cha msiba wake. Nawapa pole sana wanamuziki na mashabiki wake na dunia kwa ujumla baada ya kifo cha mwana muziki Michael Jackson kufariki
dunia, alikuwa Pele akaja Maradonna akaja Zidane kufa yeye kusiwe ndio mwisho wa muziki wa pop atakuja Akon na wenginewe.
Mungu ailaze pema roho yake. Kila kitu kina mwanzo na mwisho na huu ndio mwisho wake Michael Jackson tumuombee dua mungu ampumzishe pahala pema "Ameen". Mimi kitu ninacho kumbuka ni kwamba kijana huyu aliyefariki dunia alikuwa shujaa, kwa sababu ni kijana aliyekuwa kafanikiwa
kimaisha kwa ajili ya jasho lake haitoshi kazaliwa katika familia dunia, pamoja na kashfa nyingi tu zilizomkumba alikuwa bado
ni kipenzi cha watu.
Mungu amlaze pema Michael Jackson.Tukiachana na mimi Wako Jacko atakumbukwa na dunia nzima. Nachokumbuka toka Jacko ni jinsi alivyokuwa akicheza, hivyo kaka yangu alikuwa ananivisha kama Jacko ili nicheze, hakika si mimi tu ambaye nilikuwa nauiga mtindo huo wa marehemu Jackson bali wengi tu,haswa huku Tanzania. Kusema kweli ni pengo kubwa aliloacha. Nakumbuka mengi tu kuhusu Jacko wakati nilipopewa zawadi shuleni nilivyoucheza wimbo
wake unaokwenda kwa jina la 'You Rock Ma World'. Pia sisahau kamwe nilivyokuwa namwaga machozi wakati Jacko alivyofikishwa mahakamani akikabiliwa na mashtaka ya ulawiti.
Buriani Michael Jackson. Kifo cha Michael Jackson kimetugusa wengi hususan sisi mashabiki wa pop, mimi binafsi nakikumbuka kibao chake cha "Thriller",
akinengua stejini kwa staili ya vidole huwa nakumbuka mbali sana. Tumuenzi kwa yale mema aliyoyatenda na tumuombe katika safari
yake ya mbinguni. Mungu amlaze mahali pema peponi Amina. Mimi nilikuwa nataka kujua je Michael Jackson kafa akiwa muislam? Kwasababu nilisikia kasilimu. Maoni zaidi BBC inatusaidia
sana hasa sisi wanafunzi hongereni kwa hilo. Michel Jackson lala salama na uanze maisha mapya kaburini. Nimepokea kwa masikitiko sana kifo cha Wacko Jacko.Ulimwengu wa muziki umempoteza mtu ambaye itakuwa ngumu kuziba pengo lake.Tutamkumbuka
Michael Jackson daima, apumzike kwa amani. Michael Jackson tulimpenda sana kwa kweli tumepoteza mtu muhimu katika ulimwengu wa pop, sijaona kama Michael na wanamuziki
wanalijua hilo. Maoni yangu tumuenzi kwa hali na mali kwa yote aliyoyafanya katika uhai wake kama vile kusaidia watoto yatima
na kupinga unyanyasaji wa haina yoyote duniani. Nimehuzunishwa sana na kifo cha aliyekuwa gwiji wa muziki wa pop duniani. Ni kweli hiki ni kipindi kigumu sana kwa familia
ya Jacko pamoja na mashabiki wake. Tunafahamu na kutambua mchango wake katika harakati za watu weusi. Ni tabia yake ya kuukana uafrika na dharau iliyopindukia ndiyo mambo ambayo daima atakumbukwa kwa hayo, ukiacha hayo ni mwanamuziki
aliyekuwa wa viwango vya juu kabisa aliyepata kuishi katika karne ya 20.Jina la Bwana lihimidiwe. Tunasitika nasikitika kumpoteza Michael Jackson tutamkumbuka kumpoteza Michael Jackson tutamkumbuka uchezaji wake mahiri wa
muziki wa pop.
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||