|
Picha za Faidika na BBC
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
Washindani wa Faidika na BBC 2008, kutoka kushoto Witness Omoga [Kenya], Apolinary Joseph Laksh [Tanzania], Ashura Kisesa [Burundi - mshindi], Derick Kajukano [Uganda] na Rangira Aime Frederick [Rwanda].
Mshindi wa Faidika na BBC, Ashura Kisesa akiwa na meneja wa Faidika na BBC, Salim Kikeke.
Meneja wa Faidika na BBC, Salim Kikeke akizungumza "live" kwenye Dira ya Dunia wakati wa kutafuta mwakilishi wa Burundi katika Faidika na BBC 2008, aliyeshikilia kinasa sauti ni Ramadhani Kibuga mwandishi wetu wa Burundi.
Tom Japanni, al maarufu wa kipindi cha Kimasomaso akiwa na mtangazaji mwenzake Amina Aboubakar, wakifanya mazoezi ya kurusha Faidika na BBC 2008 kutoka Kampala, pembezoni ni Solomon Mugera, mkuu wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC akiwatupia jicho.
Salim Kikeke, meneja wa Faidika na BBC 2008 akifichua tuzo iliyotolewa kwa mshindi wa 2008.
Jaji Madina Juma wa Rwanda akitangaza mshindi wa kitaifa, mwenye fulana nyeusi ni Yves Bucyana mwandishi wa BBC nchini Rwanda.
Arnold Kweka, kutoka Tanzania, mmoja wa majaji akihojiwa na Anne Mawathe katika matangazo ya BBC baada ya mshindi kupatikana. |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||