|
BBC Ulimwengu wa Soka
|
||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
Idhaa ya Kiswahili ya BBC ikishirikiana na redio washirika, Jumamosi ya tarehe 03 mwezi Oktoba 2009, tutakuletea moja kwa
moja matangazo ya mechi ya ligi kuu ya Premier ya England, kati ya Bolton na Tottenham Hotspurs.
Mechi hiyo itaanza saa 1700 za Afrika Mashariki, lakini kumbuka matangazo ya Ulimwengu wa Soka yanaanza saa 1630. Mechi zaidi za wikendi hiyo kwa saa za Afrika Mashariki; Jumamosi, 03 Oktoba 2009 Bolton v Tottenham, 17:00 Jumapili, 04 Oktoba 2009 Arsenal v Blackburn, 15:30 Jumatatu, 05 Oktoba 2009 Aston Villa v Man City, 22:00 Unaweza kutoa maoni yako kwenye BBC Ulimwengu wa Soka kwa kutuandikia ujumbe mfupi wa maandishi, yaani text message au SMS,
ukitumia nambari hii: + 44 7786 202 005. Kombe la Dunia kwa Watoto Wanaozurura Mitaani 2010 Tanzania ni miongoni mwa mataifa ambayo yatashirikishwa katika mashindano ya soka ya Kombe la Dunia, kwa vijana wanaozurura ovyo mitaani, yatakayofanyika mjini Durban, Afrika Kusini, mwezi Machi mwaka 2010. Mbali na wenyeji, mataifa mengine yatakayoshiriki ni Brazil, India, Nicaragua, Ufilipino, Ukraine, Uingereza na Vietman. Jumanne ya tarehe 22 Julai 2009, meneja wa chuo cha michezo cha watoto kutoka Mwanza,Tanzania, Bw Mutani Yangwe, alishiriki katika kikao mjini London kuzungumzia juu ya mashindano hayo ya dunia, na vile vile juu ya mipango ya Arsenal, klabu ya Uingereza, kukisaidia chuo hicho. |
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||
|
|||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||||