bbc.co.uk navigation

Villas-Boas ahofia hatma yake

Imebadilishwa: 28 Februari, 2012 - Saa 19:18 GMT

Meneja wa Chelsea Andre Villas-Boas ahofia hatma yake

Kocha wa Chelsea Andre Villas-Boas amekiri kwamba anahofia majaaliwa yake katika klabu hiyo.

Villas-Boas, mwenye umri wa miaka 34, siku zote amesisitiza kuwa anaungwa mkono na mmiliki wa Chelsea Roman Abramovich.

Lakini katika mahojiano na kituo kimoja cha redio cha nchini Ureno anasema huenda akatimuliwa kama Carlo Ancelotti, ambaye alifutwa kazi mwezi Mei mwaka jana.

"Sijui kama nitakuwa hapa kesho au miaka miwili kutoka sasa, inategemea mtu anaelewa vipi hali ilivyo" alisema Villas-Boas.

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.