bbc.co.uk navigation

Senegal yaombwa itulie

Imebadilishwa: 25 Februari, 2012 - Saa 18:24 GMT


Viongozi wa kimataifa wameisihi Senagal kuwa tulivu kabla ya uchaguzi wa Jumapili, ambapo Rais Abdoulaye Wade anagombea muhula wa tatu wa uongozi.

Mfuasi wa Rais Wade kwenye kampeni

Uamuzi wa kiongozi huyo wa miaka 85, wa kugombea tena urais kinyume na katiba iliyoweka mihula miwili tu, umezusha maandamano ya majuma kadha.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban ki-Moon, ametoa wito wa uchaguzi wa amani na wa kuaminika.

Rais wa sasa wa Umoja wa Afrika - Thomas Boni Yayi wa Benin - amewasihi watu wa Senegal wasahau hitilafu zao.

Taarifa zinazohusiana

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.