bbc.co.uk navigation

Waandishi habari wauawa Syria

Imebadilishwa: 22 Februari, 2012 - Saa 12:41 GMT
Marie Colvin mwandishi habari wa Marekani

Serikali ya Ufaransa imethibitisha kwamba waandishi habari wawili wa kimataifa wameuawa katika mji wa Homs, Syria.

Msemaji wa serikali amesema waliokufa ni pamoja na Marie Colvin mwandishi wa kimataifa kutoka Marekani pamoja na mpiga picha raia wa Ufaransa Remi Ochlik. Bi Colin alikuwa mwandishi wa gazeti la Sunday Times huko Marekani.

Wanaharakati wa Syria wamesema wawili hao walikufa baada ya kombora kupiga nyumba walimokuwa wakipeperushia matangazo yao eneo la Baba Amr.

Kwenye ripoti yake hapo Jumanne Colvin alisema mashambulizi ya jeshi la serikali yalifanywa bila kujali usalama wa raia.

Mwanaharakati wa Syria ambaye amekuwa akitoa kanda za video pia aliuawa mjini Homs.

Taarifa zinazohusiana

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.