bbc.co.uk navigation

Jeshi la Nigeria lawauwa Boko Haram

Imebadilishwa: 21 Februari, 2012 - Saa 02:13 GMT

Msemaji wa jeshi la Nigeria amesema kwamba wanajeshi watatu walijeruhiwa katika

makabiliano hayo ya risasi na kundi la Boko Haram.

Walinda usalama katika mji wa Maiduguri

Hata hivyo alikanusha kuwa kuna raia yeyote aliyeuwawa katika kisa hicho.

Lakini wenye maduka katika soko la Baga wamenukuliwa wakisema kuwa wameona maiti zipatazo ishirini hivi zikipakiwa kwenye lori.

Eneo hilo la Maiduguri ni ngombe kuu ya wapiganiaji wa Boko Haram . Na katika miaka ya hivi karibuni sehemu imeshuhudia milipuko kadhaa na ufyatuliananji wa risasi.

Tayari serikali ya rais Goodluck Jonathan imetangaza hali ya hatari katika mji huyo na miji menginea ambayo imeshuhudia mashambulizi toka kwa kundi hilo la Boko Haram.

Lakini wakazi wa miji hiyo wanasema kuwa suluhu ya kijeshi haijafaulu leta mafanikio yeyote

Taarifa zinazohusiana

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.