bbc.co.uk navigation

Vikwazo vyaiumiza Syria

Imebadilishwa: 19 Februari, 2012 - Saa 09:37 GMT

Mfanya biashara mmoja maarufu wa Syria anasema uchumi wa nchi hiyo unaumia kwa sababu ya vikwazo vya kiuchumi vilivowekwa na nchi nyengine dhidi ya Syria na kwamba Rais Bashar al-Assad na serikali yake haikuelekea kuweza kudumu zaidi ya miezi sita.

Jeshi la Syria

Faisal al-Qudsi, mtoto wa rais wa zamani wa Syria, aliiambia BBC kwamba vikwazo dhidi ya mafuta ya Syria na utalii kupotea, kumepunguza pato la taifa kwa asili-mia-45.

Alisema serikali ya Syria inapata pesa kutoka Iran lakini hazitoshi na wafanya biashara wa Syria wameacha kumuunga mkono Rais Assad.

Alisema wafanya biashara wengi wanahofia maisha yao na wameondoka nchini.

Taarifa zinazohusiana

BBC © 2012 Ilani: BBC haihusiki na yaliyoandikwa na tovuti za nje ya BBC.

Ukurasa huu unaonekana vyema kwa kivinjari cha kisasa kikiwa na laha mtindo (CSS).Wakati unaweza kuona yaliyomo katika ukurasa huu kwa kivinjari ulichonacho, hautaweza kufaidi kuona kila kitu vizuri. Tafadhali zingatia uwezekano wa kuboresha progaramu ya kivinjari au kuwezesha laha mtindo (CSS) endapo unaweza kufanya hivyo.