Mfanya biashara mmoja maarufu wa Syria anasema uchumi wa nchi hiyo unaumia kwa sababu ya vikwazo vya kiuchumi vilivowekwa na nchi nyengine dhidi ya Syria na kwamba Rais Bashar al-Assad na serikali yake haikuelekea kuweza kudumu zaidi ya miezi sita.

Faisal al-Qudsi, mtoto wa rais wa zamani wa Syria, aliiambia BBC kwamba vikwazo dhidi ya mafuta ya Syria na utalii kupotea, kumepunguza pato la taifa kwa asili-mia-45.
Alisema serikali ya Syria inapata pesa kutoka Iran lakini hazitoshi na wafanya biashara wa Syria wameacha kumuunga mkono Rais Assad.
Alisema wafanya biashara wengi wanahofia maisha yao na wameondoka nchini.